Namba ya usajili: S4524 Kituo cha mitihani: S 4810 P4809
S.
L. P 264 Kasulu – Kigoma – Tanzania
Simu:
0767 322707/ 0756 555 011 / 0752 486 955,
Barua
pepe: magabasecondary@gmail.com
Mahali
shule ilipo ni Kasulu barabara ya Kibondo Jirani na Kijiji cha Nyakitonto.
MAELEKEZO
YA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2023.
Jina
la mwanafunzi. ____________________________________________
Uongozi
wa Shule ya Sekondari Magaba unapenda kukutaarifu kwamba umekubaliwa kujiunga
na Kidato cha kwanza katika Shule hii kwa mwaka wa masomo 2023. Magaba
Sekondari ni Shule ya bweni tu kwa wavulana na wasichana; Shule ipo Wilaya ya
Kasulu, Mkoani Kigoma umbali wa kilometa ishirini toka Kasulu mjini barabara
iendayo Mwanza (Kibondo Road).
Shule
itafunguliwa tarehe 07 Januari 2023 siku ya Jumamosi hivyo unapaswa kuwahi
mapema shuleni kabla ya saa kumi jioni.
Magaba
Sekondari ni Shule iliyosajiliwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa
namba S4524, namba ya kituo cha
Mtihani wa Taifa ni S4810 na namba
ya kituo kwa wanafunzi wa kujitegemea (Private
Candidates) ni S4809.
Shule
inafundisha masomo yote ya msingi ambayo ni:-
Civics, History, Geography, Kiswahili, Englisha Language,
Physics, Chemistry, Biology, Basic Mathematics na Literature in English.
Maabara zote za masomo ya
sayansi zipo, tunao walimu wa masomo yote wenye uzoefu wa kutosha na
wachapakazi. Maadili yanafundishwa kupitia elimu ya dini Shuleni kwa madhehebu
yote. Uhuru wa kuabudu unapewa kipaumbele kwa siku husika na dhehebu husika na
ibada za kila siku jioni zinazingatiwa na kusimamiwa ipasavyo.
Unatakiwa kusoma na
kuelewa sharia na taratibu za shule. Pia utajaza fomu zote, F. 01, F. 02 na F.03
kama zinavyoelekeza na kuzileta shuleni siku ya kuripoti. Fomu hizi
zimeambatanishwa na barua hii.
Unatakiwa kujaza fomu
zote, F1, F2 na F3 na kuzileta shuleni siku ya kuripoti. Fomu hizi
zimeambatanishwa na barua hii.
KARIBU SANA MAGABA SEKONDARI KWA ELIMU BORA.
Wako
katika elimu
-------------------------
Mkuu
wa Shule
1. 0
ADA
(KARO) NA MAHITAJI YA SHULE:
Ada ya
Shule ni shilingi za Kitanzania 1, 300, 000/=
(million moja na laki tatu tu)
1. 1 ADA INALIPWA KWA AWAMU NNE
KAMA IFUATAVYO:-
·
Januari
500, 000/=
·
Aprili
200,000/=
·
Julai 400, 000/=
·
Septemba
200, 000/=
1.2 MICHANGO MINGINE
Huduma ya kwanza na uthibiti ubora wa shule
pamoja na UMISETA ni Tsh.50, 000/=
Ada ya shule tu ndiyo ilipwe kwenye mojawapo
ya akaunti za Shule, aidha kupitia
NMB
A/C NO: 51410004076 au CRDB A/C NO: 0150227648600
Jina
la akaunti zote ni MAGABA SECONDARY SCHOOL.
Mwanafunzi atakapolipa aje na Bank Pay in
slip ya malipo ya ada shuleni.
Pay in slip iandikwe jina la mwanafunzi na
kidato chake na si jina la mzazi / mlezi aliyeweka fedha benki. Michango yote ikiwa ni
pamoja na ada za mitihani ya kitaifa na mock iletwe taslimu shuleni.
2.0
MAHITAJI MUHIMU;
TAALUMA
·
Oxford
Student Dictionary: For learners using English to Study other subjects.
·
Ream
mbili (02) A4 za karatasi nyeupe kwa ajili ya photocopy kwa mwaka mzima.
·
Ream moja
(01) Ruled papers karatasi za misitari – Kidato cha 3 na 4 tu
·
Spring
files mbili (2) (Moja kwa ajili ya kutunzia mitihani yake na jingine litakabidhiwa
kwa mkuu wa shule kwa ajili ya taarifa binafsi za mwanafunzi)
·
Graph
Pad Paper moja
·
Kitabu
Student’s Companion by Wilfred Best
·
Biblia
/ Quran (Kadri ya Imani)
·
Four
Figure (Mathematical tables)
·
Note book
kwa ajili ya Nukuu (Summary) moja kwa kila somo
·
Rula
ndefu (Futi moja)
·
Mkebe
wa Hisabati (Mathematical Set)
·
Kalamu
za wino za kutosha, Penseli na kifutio
·
Vitabu
angalau viwili vya masomo yoyote kwa kidato husika – (ni mali ya mwanafunzi)
·
Daftari
za kutosha masomo yote zisizopungua 12 (Counter Book Q3 au 4)
MUHIMU: Vifaa
vyote hivi vinapatikana kwenye duka la Shule. Tunashauri mwanafunzi anunue
vifaa tajwa hapo juu hapahapa shuleni kwa bei nafuu kabisa ambayo si tofauti na
ile ya Kasulu mjini. Hii itasaidia kuepuka kununua vifaa tofaiti na mahitaji ya
shule. Lakini pia itakupunguzia usumbufu wa kusafiri na mizigo mingi.
2.1. SARE ZA SHULE.
2.1.1.
WAVULANA
-
Suruali
mbili za rangi ya zambarau kitambaa kizito (Istimu) Suruali ziwe za heshima na
zisiwe za kubana, ziwe na marinda.
-
Mashati
mawili meupe mikono mifupi
-
Viatu
vyeusi jozi mbili siyo vya visigino virefu
-
Soksi
ndefu pea mbili au zaidi rangi nyeusi
-
Mavazi
ya michezo; Viatu vya michezo, Bukta na Tshirt ya rangi ya bluu
-
Nguo
za kuvaa baada ya masomo (au za kushindia) Suruali 2 nyeusi za kitambaa na siyo
mtumba ziwe za heshima
-
Tshirt
mbili (2) zinaptikana shuleni (30,000)
-
Truck
suit rangi ya Kijani jeshi
-
Sweta
rangi ya damu ya mzee.
-
Brash
ya Viatu, Kiwi au dawa ya viatu nyeusi
-
Mkanda
mweusi wa ngozi
-
Nguo
za ndani za kutosha
-
Shuka
jozi mbili za rangi ya bluu bahari (Light bluu)
-
Blanketi,
mto wa kulalia na foronya
-
Chandarua
cha mbu, kiwe kipya
-
Mafuta
ya kujipaka
-
Sanduku
la chuma (Trunk) na kufuli zake
-
Sabuni
za kufulia na kuogea za kutosha
-
Taulo
-
Kandambili
/ yeboyebo
-
Dawa
ya meno na miswaki (3)
-
Tochi
ya betri kwa ajili ya dharura wakati umeme unapokuwa umekatika kabla ya kuwasha
jenereta
-
Godoro
la futi 2½ (Dodoma QFL) au kukodi godoro la shule Tsh. 10,000/- kwa kila muhula.
-
Vyombo
vya kulia chakula (Sahani, Bakuli, Kikombe na Kijiko)
-
Dumu la
lita 5 la kutunzia maji ya kunywa.
Angalizo: Vifaa vyote viwekewe alama binafsi ya
utambulisho
2.1.2. WASICHANA
-
Sketi
mbili zenye malinda mapana rangi ya zambarau kitambaa kizito, Sketi ziwe ndefu,
zifike chini ya magoti sketi fupi haziruhusiwi.
-
Shati
mbili za mikono mifupi
-
Viatu
vyeusi jozi mbili siyo vya visigino virefu
-
Mavazi
ya michezo: Tshirt rangi ya bluu, Sketi ya Kitambaa cha Sukarisukari rangi
nyekundu.
-
Nguo
za kuvaa baada ya masomo (au za kushindia) gauni mbili za malinda rangi ya dark
bluu zinapatikana shuleni kwa gharama ya Tshs 40,000/= @
-
Brashi
ya viatu, Kiwi au dawa ya viatu vyeusi
-
Nguo
za ndani za kutosha
-
Taulo
za kike (Pedi)
-
Shuka
jozi mbili rangi ya bluu bahari (Light blue)
-
Blanketi,
Mto wa kulalia na foronya
-
Chandarua
cha mbu, Kiwe kipya
-
Mafuta
ya kujipaka
-
Sanduku
la chuma (Trunk) na kufuli zake
-
Sabuni
za kufulia na kuogea za kutosha
-
Tshirt
mbili (2) zinapatikana shuleni (30,000/=)
-
Truck
suit rangi ya kijani zinauzwa shuleni (30, 000/=)
-
Sweta
rangi ya damu ya mzee zinauzwa shuleni (10, 000/=)
-
Taulo na
khanga
-
Kandambili
/ yeboyebo
-
Dawa
ya meno na miswaki 3
-
Tochi ya
betri kwa ajili ya dharura wakati umeme unapokuwa umekatika kabla ya kuwasha jenereta
ya shule
-
Godoro
la futi 2½ (Dodoma QFL) au kukodi godoro la shule Tsh. 10,000/- kwa kila
muhula.
-
Vyombo
vya kulia chakula (Sahani, Bakuli, Kikombe na Kijiko)
-
Dumu
la lita 5 la kutunzia maji ya kunywa yaliyochemshwa
Angalizo:
Vifaa vyote viwekewe alama binafsi ya
utambulisho
2.2 VIFAA
VYA USAFI
i.
Ndoo
na mfagio (Mopa)
ii.
Ndoo
ndogo lita 10
iii.
Mfagio
(squeezer)
iv.
Mfagio
wa nje (chelewa)
v.
Beseni
vi.
Mpini
wa jembe la mkono
3.0 VITU VISIVYOTAKIWA SHULENI
i.
Aina
yoyote ya manukato (Perfume), Lotion au Vipodozi vyovyote vya kujichubua.
ii.
Simu,
Radio, Camera, Mishumaa, Mapambo kama vile hereni, Pete na Mikufu.
iii.
Vitu
vyenye ncha kali kama Kisu, Sindano na kadhailika.
4.0
AFYA
Mtoto
anatakiwa afanyiwe uchunguzi wa afya kwa daktari wa Hospitali inayotambulika na
Serikali. Vielelezo vya afya yake vijazwe kikamilifu kwenye fomu kisha aje na
fomu hiyo. Aidha, mtoto mwenye matatizo mengine ya afya aje na vyeti vya
udhibitisho na kumbukumbu, fomu ya afya imeambatanishwa na maelekezo haya ya
kujiunga na Shule.
Sharti
la lazima mtoto awe na Bima ya Afya
ama ya jamii iliyoboreshwa (CHF) au ya Taifa (NHF) kwa wale ambao ni wafaidika
wanaohudumiwa na Serikali. Shule inatoa huduma ya kwanza tu. Tujenge utamaduni
wa kupima afya kila mara kwa watoto wetu hasa kila wanapokuwa likizo.
5.0
UTUNZAJI WA MALI ZA SHULE.
Mwanafunzi
atawajibika kutunza vifaa vyote atakavyopewa kutumia shuleni. Yeyote
atakayeharibu mzazi / mlezi atawajibika kulipa au kutengeneza uhalibifu
utakaokuwa umesababishwa na mwanafunzi husika.
Mwisho
shule inakukaribisha sana hapa Magaba Sekondari ili ushiriki kikamilifu katika
kukuza vipaji vyako ili vikuwezeshe kuwa Raia mwema na kukua katika Maadili,
Uzalendo, Udadisi na Utayari katika kumudu maisha yako na changamoto za
kimaisha mbeleni.
KARIBU
SANA MAGABA SEKONDARI
MAWASILIANO: 0767 322707, 0784 555011, 0765
801000
Wako
katika elimu
-------------------------
Mkuu wa Shule.
SHULE YA SEKONDARI MAGABA
S. L. P. 264, KASULU TANZANIA
TARATIBU ZA SHULE
1.0
SHERIA
NA MASHARTI YA SHULE
Kila
mwanafunzi aliyechaguliwa kujiunga au kuhamia lazima apime afya yake na kujaza
fom iliyoambatanishwa na maelekezo haya na kuirudisha shuleni. Fomu hii ijazwe
na Daktari wa serikali mwenye cheo cha Clinical Officer au Medical Officer na
kupigwa muhuri.
1.1
TAALUMA:
Lengo
la shule ni kuwa kitovu cha taaluma na nidhamu bora na hatimaye kuwa shule bora
katika mkoa wa Kigoma na Tanzania kwa ujumla. Dhima ya shule ni kujenga
mazingira bora ya kielimu yanayoheshimu na kujari mahitaji ya watu wote, ili
kwamba wanafunzi wetu waweze kupata stadi za kazi zitakazowawezesha kukabiliana
na changamoto za kimaisha. Ili kuyafikia haya, kila mwanafunzi hana budi kutimiza
na kutekeleza masharti yafuatayo;
a) Kila
mwanafunzi ahudhurie masomo kwa muda wa siku mia moja tisini na nne (194) kwa
mwaka, ukiondoa Jumamosi, Jumapili na sikukuu za kitaifa.
b) Kama
kutakuwa na sababu za msingi za mwanafunzi kutofika shuleni wakati wa kufungua
shule, ni jukumu la mzazi/mlezi kufika mwenyewe kutoa taarifa kwa mkuu wa shule
au kutoa taarifa ya maandishi kwa uongozi wa shule, mapema iwezekanavyo.
c) Kila
mwanafunzi awe ameingia darasani na kukaa katika kiti chake kabla yamwalimu wa
somo kuingia na kuanza kufundisha.
d) Mwalimu
aingiapo darasani wanafunzi wote wasimame na kumsalimia.
e) Wanafunzi
wote wawe kimya wakimsikiliza mwalimu wakati akifundishaisipokuwa mwalimu
akiuliza swali, akiruhusu mjadala au maigizo darasani.
f) Kila
mwanafunzi ahudhurie vipindi vyote kwa mujibu wa ratiba ya siku.
g) Kila mwanafunzi afanye mazoezi na mitihani
yote anayopewa na walimu wamasomo mbalimbali katika muda aliopewa.
h) Kila
mwanafunzi afikie wastani wa asilimia arobaini na tano (45%), kilamwisho wa
mwaka wa masomo. Mwanafunzi atakayeshindwa kufikia kiwangohicho, atalazimika
kukariri darasa
i) Mwanafunzi
yeyote ambaye atakwepa kufanya mitihani au zoezi la somololote la kidato husika
bila ruhusa iliyoidhinishwa na Mkuu wa shule, hatapewaalama yoyote na badala
yake ataandikiwa sifuri katika somo hilo na alama hiyo itajumlishwa katika
kutafutawastani wake wa mwisho wa muhula au mwaka.
j) Mwanafunzi
haruhusiwi kuibia mitihani kutoka kwa mwanafunzi mwenzake au kwenda chumba cha
mtihani na majibu yaliyoandikwa kwenye karatasi, nguo rula n.k. au kuongea na
mwanafunzi mwenzake kwenye chumba chamitihani wakati mtihani ukifanyika. Atakayebainika
kukiuka sheria hii ya shule, atapata adhabu ya kusimamishwa masomo na hatimaye
kufukuzwa shule.
k) Kila
mwanafunzi awe na daftari la mazoezi/majaribio kwa kila somo.
2.0 NIDHAMU
Shule
ya sekondari Magaba inaamini kuwa Nidhamu Bora ni Ufunguo wa Taaluma Bora. Kwa
hiyo, inahimiza sana juu ya umuhimu wa wanafunzi kuwa na nidhamu bora. Kama
sehemu ya nidhamu bora, kila mwanafunzi anapaswa:
a)
Awe amefika Smart area kabla ya saa moja na dakika ishirini asubuhi akiwa
katika sare rasmi ya shule iliyo safi.
b)
Awahi kuhudhuria Mkutano wa Asubuhi na
mchana (School Assembly) au mikutano ya asubuhi ya darasa kwa siku na wakati
husika.
c)
Awepo mahali husika kwa mujibu wa ratiba ya
siku hiyo.
3.0 AFYA NA USAFI
Afya na Usafi ni sehemu
muhimu ya Taaluma na Nidhamu bora. Kwa hiyo, ni lazima: -
a)
Kila mwanafunzi aonekane nadhifu wakati
wote.
b)
Mwanafunzi ashiriki katika kusafisha na
kutunza mazingira ya shule ikiwa ni pamoja na kufagia /kudeki vyumba vya
madarasa, kuondoa buibui, kufuta vumbi kwenye vioo, milango, madirisha n.k.
kila atakapotakiwa kufanya hivyo.
c) Kila
mwanafunzi atunze vifaa vya kufanyia Usafi, atakavyokabidhiwa. Upotevu au
uharibifu wa vyombo hivyo utagharimiwa na mwanafunzi ambaye atakuwa amehusika
na uharibifu au upotevu wa vifaa hivyo.
4.0 TABIA NA MWENENDO
Kila mwanafunzi anatakiwa afanye yafuatayo:
a)
Mwanafunzi anatakiwa kuwasalimu wafanyakazi
wote wa shule atakaokutana nao ndani na nje ya shule.
b)
Wanafunzi wote wanapaswa kuheshimu,
kusimama kwa ukakamavu, kuwa kimya wakati wimbo wa taifa unaimbwa na wakati
bendera ya taifa inapopandishwa au kuteremshwa.
c)
Mwanafunzi anatakiwa kupokea /kutii amri
zote halali zitolewazo na utawala wa shule bila ubishi.
d)
Mwanafunzi HARUHUSIWI kutumia lugha
ya matusi.
e)
Ni marufuku kupiga kelele au kuleta
usumbufu wa aina yoyote bwenini, darasani au nje ya darasa.
f)
Ni marufuku mwanafunzi kutoka nje ya shule
wakati wa masomo bila ya ruhusa toka kwa Mkuu wa shule au waandamizi wake.
g)
Kila mwanafunzi atawajibika kutunza mali
yake binafsi pamoja na ile ya shule na kutoa taarifa kwa utawala wa shule
endapo mali hizo zitaharibiwa/kuibiwa.
h)
Mwanafunzi haruhusiwi kuja shuleni na vitu
vya thamani kubwa vinavyoweza kuathiri tabia na mwenendo wake kitaaluma na
kinidhamu; kama vile simu za mkononi, redio, kamera, sistimu ya video, kompyuta
ndogo (laptops) au fedha nyingi kuliko mahitaji yake.
i)
Ni marufuku mwanafunzi kuiba mali ya
mwenzake au ya shule.
5.0 SHERIA ZA BWENI
a)
Zungumza lugha ya Kiingereza wakati wote
b)
Kupiga kelele hairuhusiwi
c)
Dumisha usafi bwenini
d)
Tandika kitanda chako na kuhakikisha ni
kisafi daima
e)
Hakikisha mabomba ya maji yamefungwa na
hayatoi maji ovyo. Pia hakikisha taa zote zimezimwa pale ambapo hazihitajiki
kwa wakati huo.
f)
Weka vifaa vyako kwenye begi na sanduku
lako
g)
Usitundike nguo zako ukutani, kitandani
wala dirishani
h)
Weka viatu vyako kwa mpangilio chini ya
kitanda chako
i)
Lala kwenye kitanda ulichopewa tu na siyo
vinginevyo
j)
Redio haziruhusiwi bwenini
k)
Simu za mkononi (mobile phones)
haziruhusiwi shuleni/bwenini
l)
Vaa nguo za heshima uwapo bwenini na hasa
nguo zilizoruhusiwa
m)
Mapambo na vitu vingine kama mikufu, shanga
nk haviruhusiwi
n)
Hairuhusiwi kuandika maandishi yoyote
ukutani.
o)
Hairuhusiwi kununua vyakula vya aina yoyote
kutoka nje ya maeneo yanayolizunguka bweni
p)
Lugha ya matusi hairuhusiwi ndani na nje ya
bweni
q)
Hairuhusiwi kunywa kileo cha aina yoyote,
kuvuta sigara au madawa ya kulevya.
r)
Hairuhusiwi kuvunja au kuharibu kitu
chochotekilicho mali ya bweni (shule)
s)
Hairuhusiwi kulala bwenini kwa kuumwa bila
kibali cha matron au patron wa shule.
t)
Hairuhusiwi kulala wanafunzi zaidi ya mmoja
kwenye kitanda kimoja
u)
Hairuhusiwi kulala kwenye kitanda kisicho
chako.
v)
Hakuna mwanafuzni atakayeruhusiwa kwenda
nje ya eneo la shule bila ruhusa ya Mkuu wa shule.
w)
Wakati wa kusafiri, kila mwanafunzi atavaa
sare za shule.
x)
Vifaa vyote atakavyokuja navyo mwanafunzi
vitakaguliwa wakati wa udahili.
y)
Chakula toka nje hakiruhusiwi shuleni.
Wanafunzi wote watakula chakula kitakachotolewa shuleni.
MAKOSA YAFUATAYO NI YA KUMFUKUZA MWANAFUNZI
SHULENI.
i.
Kupiga / Kupigana
ii.
Wizi wa kila aina, iwe wa kutumia nguvu au
udanganyifu.
iii. Uasherati
na kila aina ya tabia inayohusiana na mahusiano ya kimapenzi.
iv. Ulevi
wa aina yoyote na uvutaji wa sigara / bangi / kuberi na kadhalika.
v.
Makosa ya jinai
vi. Kuharibu
kwa makusudi mali za umma / shule / mwanafunzi
vii. Kudharau
alama za Taifa (Bendera na Wimbo wa Taifa)
viii. Kusababisha,
Kubeba au kutoa mimba / kuwa mjamzito au kusababisha ujauzito ndani au nje ya
shule.
ix. Kuoa
au kuolewa / kuwekwa kimada /ushoga
x.
Utoro wa mfululizo
xi. Wizi
wa mitihani
xii. Aina
yoyote ya uonevu kwa mwanafunzi mwenzako
xiii. Kutumia
lugha chafu kwa Wafanyakazi /wanafunzi wenzako
xiv.
Kutoka nje ya shule au kuingia shuleni bila
taarifa yoyote
xv.
Kutoroka shuleni mchana na usiku / kuruka
ukuta au uzio kutoka nje ys shule
xvi.
Kuingia katika majumba ya starehe
xvii.
Kuwa na Simu/ Redio uwapo shuleni
xviii.
Kugoma na kuvuruga amani na usalama wa watu
shuleni
ANGALIZO
·
Sheria hizi zimetungwa kwa mujibu wa sheria
za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa mujibu wa Wizara ya Elimu, na Mafunzo
ya Ufundi.
·
Pia, sheria zote zinalenga kumjenga
mwanafunzi kiakili na kimaadili ili hatimaye aweze kulitumikia Taifa kwa
uadilifu na kuwa raia mwema.
·
Sheria nyingi za bweni hutungwa kufuatana na
sheria za nchi. Aidha baadhi ya sheria hutungwa kwa kuzingatia mazingira ya
shule na kanuni za wizara ya Elimu zinazohusu uendeshaji wa Shule za Sekondari.
Kila mwanafunzi anapaswa kuzisoma na kuzielewa sheria hizo kwa nia ya
kuzifuata.
·
Uvunjaji wa sheria za shule unaweza
kusababisha mwanafunzi kupewa adhabu au kufukuzwa shule
·
Utii wa kengele ni jambo muhimu sana kila
mwanafunzi anahimizwa azingatie.
·
Sheria hizi zina lengo la kuleta amani na
utulivu shuleni hivyo kila mwanafunzi ni lazima azifuate.
Wako katika elimu
-------------------------
Mkuu wa Shule.
(Sheria
za shule hizi ni nakala ya mwanafunzi na anapaswa abaki nazo na azisome mara
kwa mara ili azielewe na kuziishi)
F. 01
MAGABA SECONDARY SCHOOL
MEDICAL EXAMINATION FORM
(To be
filed by an Authorized Government Medical Officer and returned to school)
TO THE MEDICAL OFFICER
__________________________________________________________________________________
__________________________________________________________________________________
__________________________________________________________________________________
RE: Master / Miss
___________________________________________________________________
Please examine the
above student as to her/his physical fitness for a full time schooling course.
The examination should include categories a - n. Each category of which will render
the applicant ineligible of defect.
MEDICAL CERTIFICATE
_____________________________________________
have examined the above subject and consider that he / she is physically fit /
unfit for a full time schooling course.
(a) Eye sight ________________________________________________________________________________
(b) Hearing _________________________________________________________________________________
(c) Limbs __________________________________________________________________________________
(d) Speech _________________________________________________________________________________
(e) Venereal Disease __________________________________________________________________________
(f) Leprosy _________________________________________________________________________________
(g) Epilepsy ________________________________________________________________________________
(h) Asthma _________________________________________________________________________________
(i) Heart Problem ____________________________________________________________________________
(j) Kidney __________________________________________________________________________________
(k) Peptic Ulcers _____________________________________________________________________________
(l) Sickle cell anemia _________________________________________________________________________
(m)
TB ____________________________________________________________________________________
(n) Chronic Malaria __________________________________________________________________________
(o) Neurosis ________________________________________________________________________________
(p) Other serious disease ______________________________________________________________________
Date _________________________________ Signature _____________________
Official stamp of
the Hospital Designation
___________________
(Fomu hii iikabidhiwe shuleni kwa mkuu wa shule kwa ajili ya
matumizi ya ofisi)
F. 02
SHULE YA SEKONDARI MAGABA
S. L. P
264, KASULU TANZANIA
FOMU YA
KUORODHESHA NDUGU WATAKAOMTEMBELEA MTOTO SHULENI
Ndugu mzazi / mlezi _________________________________________________________
Shule ya Sekondari Magaba inakutaarifu kuwa mwanao
atakapojiunga na shule hii atapewa muda wa kuonana na kuongea na ndugu zake kwa
muda utakaopangwa. Itapangwa tarehe maalumu toka kwa 0fisi ya Mkuu wa shule.
Kwa hiyo, shule hii inapenda kuwafahamu ndugu watakaomtembelea mwanao akiwa
shuleni. Uongozi wa shule unakushauri uwachague kwa makini na uwaorodheshe
katika fomu hii. Fomu hii lazima irudishwe shuleni kwa ajili ya utekelezaji wa
maadili ya vijana.
No. |
JINA |
UHUSIANO |
1 |
|
|
2 |
|
|
3 |
|
|
4 |
|
|
Mimi
____________________________ Mzazi / Mlezi wa ______________________________
Nimeidhinisha
watu wenye majina yaliyoandikwa hapo juu kumtembelea mwanangu kulingana na
taratibu zilizowekwa na shule ya sekondari Magaba. Mtu yeyote mwingine ambaye
hayuko kwenye orodha hii, atakuja kumtembelea mwanangu baada ya kupewa ruhusa
na mimi mwenyewe na kuujulisha uongozi wa shule. Endapo atatokea mtu yeyote
kuja kumuona mwanangu bila ruhusa yangu nijulisheni mara moja.
Namba
yangu ya simu ni ______________________________
(Fomu hii
iikabidhiwe shuleni kwa mkuu wa shule kwa ajili ya matumizi ya ofisi)
PICHA YA MWANAFUNZI
SHULE
YA SEKONDARI MAGABA
S. L. P 264, KASULU TANZANIA
MAELEKEZO.
Jaza fomu hii kwa
usahihi tumia herufi kubwa.
Fomu hii pamoja na risiti ya malipo virudishwe shuleni mwanafunzi
anapokuja kuripoti.
1. Jina la mwanafunz:i
_____________________________________________(majina matatu)
2. Tarehe ya kuzaliwa: __________________ Wilaya ___________ Mkoa: _______________
3. Sehemu anayoishi sasa ________________Wilaya:______________
Mkoa _________________
4. Dini _________________ Dhehebu ______________________________
5. Mwaka wa kumaliza darasa la saba ____________________
6. Jina la shule ya msingi
__________________________________________
7. Jina la shule ya sekondari aliyokuwa akisoma
____________________________________________
8. Jina kamili la mzazi / mlezi __________________________________________
9. Kazi ya mzazi / mlezi ________________________________________
10. Anuani ya mzazi / mlezi __________________________________
_________________________________
11. Namba ya simu ya mzazi / mlezi( kwa ajili ya mawasiliano) _____________________________
12. Barua pepe (E-mail) _______________________________________
TAMKO
LA MWANAFUNZI:
Mimi
_____________________________________ nimesoma kwa makini sheria, taratibu na
maelekezo ya shule na kuelewa. Nakubaliana na vyote na naahidi kuvifuata vyote
kwa kadiri ya uwezo wangu. Nakubali kwamba endapo nitajiingiza katika tatizo la
uvunjaji wa sheria au utaratibu wowote, hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yangu.
Jina__________________________________ Saini: ____________________ Tarehe: ______________
TAMKO LA MZAZI:
a) Mtoto
wangu akipata nafasi kujiunga na shule hii itabidi afuate taratibu, sheria na
kanuni za shule ya sekondari Magaba.
b) Ninakubali
kumlipia karo (ada) ya shule na gharama zingine anazostahili ili kumwezesha
kusoma bila tatizo, asiache masomo yake kwa ajili ya ukosefu wa mahitaji
mbalimbali.
c) Nitashirikiana
na uongozi wa shule katika kumsaidia mwanangu kitaaluma na nidhamu.
Jina
la mzazi / mlezi: _______________________ Saini:
___________ Tarehe: _____________
Namba
ya simu: ____________________________________
(Fomu hii iikabidhiwe shuleni kwa mkuu wa shule kwa ajili ya
matumizi ya ofisi)
0 comments:
Post a Comment